Wednesday 27 June 2012

Penzi ni kama kohozi

Hadija ninakuita, naomba uniitike
Kukupenda sitosita,  hata kinipiga teke
Nilini n’takupata,  nikuite wangu mke
Penzi ni kama kohozi, kulificha sitoweza

Ni weye nishaamua, mwengine sitompenda
Kila mtu kwa mtaa, yuajua nakupenda
Kupitiya i sanaa, naapa sitokutenda
Penzi ni kama kohozi, kulificha sitoweza

Alokupa u urembo, kakupa pia tabia
Sitoboi yote mambo, mengineyo takwambia
Linaua hilo umbo, bayana nawaambia
Penzi ni kama kohozi, kulificha sitoweza

Niurumie nakuomba, moyo upate tulia
Tuianze yetu nyumba, daima kufuraia
Tumshukuru Muumba, aweze kutujalia
Penzi ni kama kohozi, kulificha sitoweza

Naakika tanikithi, na jina langu ni hili
Kaburu wa Kariithi, Aderea ndo la pili
Mtungaji mwenye haathi, nayependa wana wali
Penzi ni kama kohozi, kulificha sitoweza

3 comments:

  1. Great poet in the making.Do me a favour and please maintain your posts in Kiswahili,I like!:-)

    ReplyDelete
  2. Greatly humbled Balla,I promise to n thnx alot

    ReplyDelete
  3. Lisilo budi hubidi, ewe wa Kariithi
    Fanya hala bisha hodi,takukubali amini.
    Akufae maishani, hadi pale kaburini
    Penzi ni kama sukari, limung'unye kwa ulimi.

    ReplyDelete